Nguvu YA Maneno Katika Maisha YA Mwanadamu - Joseph Nyoni Clemence - Libros -  - 9781659559675 - 12 de abril de 2020
En caso de que portada y título no coincidan, el título será el correcto

Nguvu YA Maneno Katika Maisha YA Mwanadamu

Precio
Mex$ 515
sin IVA

Pedido desde almacén remoto

Entrega prevista 28 de sep. - 14 de oct.
Recibe notificaciones sobre nuevos lanzamientos de Joseph Nyoni Clemence
Añadir a tu lista de deseos de iMusic

Aún no valorado

Nguvu ya maneno katika maisha ya Mwanadamu, ni kitabu kilichobeba uwezo wa maneno uliojificha ambao unapelekea kuathiri maisha ya Mwanadamu kupitia maneno chanya na hasi yanayoongelewa na Mwanadamu. Kitabu hiki nilianza kukiandika mwaka 2012 mwishoni, baadaye nilipokuja kufanya semina nilihamasishwa kuandika kitabu hiki ambacho nilikuwa nimepunguza kiasi ya kuandika hapo ndipo maarifa mengi yakaja na kuona kama naanza upya uandishi wa kitabu hiki cha Nguvu Ya Maneno Katika Maisha ya Mwanadamu. Kitabu hiki kimezungumzia maneno katika nyanja zote za Mwanadamu hivyo mtu yeyote asomapo kitabu hiki atajikuta akifunguka akili yake na kuona namna anavyohitaji kutumia maneno kwa jamii yake, ndugu, watoto, na marafiki bila kuacha kile anachotakiwa kujinenea yeye mwenyewe. Maneno huweza kuwa faraja kwa mtu yeyote yaani awe tajiri au masikini, na wa hali yoyote ile yaani huweza kuamsha akili ya mtu hata kuibadili kutoka katika aina ya maneno aliyoambiwa au aliyoyatumia na kuwa na misamiati mipya katika kichwa chake ambayo hutengeneza fikra mpya na Kutengeneza maisha mapya. Wakati mwingine maneno huweza kugeuka yakaleta hatari katika jamii. Kuwepo kwa ongezeko la wazazi kutoa motisha kwa watoto wao kwa kutumia maneno mazuri na hata walimu mashuleni, kunaweza kukafanya tujenge jamii mpya yenye maono na kupata wakati bora na watu kuwa bora katika nyanja zote yaani sayansi na teknolojia, uchumi, siasa, utamaduni na mengineyo kwani maneno ambayo moyo na watu wengi huweza kuamua kuyafanyia kazi yake maneno yaliyowagusa. Maneno yana athari kubwa katika jamii, na Katika karatasi za mbele nimeonyesha kwa upana kuhusu athari ya maneno kwa binadamu, kumbe basi: "Maneno safi ni njaa ya kila mtu hata awe adui wa watu maneno safi kwake ni kiu haswa, kila mmoja ana kiu ya kupata maneno safi na mazuri"Katika maeneo mengi kuna tatizo la watu wengi kushindwa kujua jinsi ambavyo maneno yanaweza kuathiri maisha yao. Sasa leo ninakuja kukueleza nikikuelimisha, nikikuhamasisha na kukufungua masikio katika fikra zako kuhusu siri ya maneno katika maisha. Kutokana na kufuatilia mambo mbalimbali ikiwemo wataalamu, kutumia fikra zangu, uzoefu wangu na mengineyo. Nimeweza kukuandalia kitabu hiki ambacho ni moja ya kitabu kilichobeba msingi wa maisha ya mwanadamu. Katika baadhi ya maeneo wapo watu ambao wamefanikiwa kunisikia nikifundisha suala hili kwa kupitia semina zangu. Haitakuwa rahisi kuwafikia watu wote hivyo ni vizuri kila mtu kwa nafasi yake aweze kupata hiki nilichonacho kupitia kitabu hiki nili

Medios de comunicación Libros     Paperback Book   (Libro con tapa blanda y lomo encolado)
Publicado 12 de abril de 2020
ISBN13 9781659559675
Páginas 218
Dimensiones 216 × 280 × 12 mm   ·   517 g
Lengua Inglés